Sheikh Abubakar Baini amesisitiza haja ya kuondoa kipengee kwenye cheti cha ndoa cha kiisalmu, kinachohitaji mwanamke kuelezea iwapo alikuwa bikara au la.
Haya yanajiri huku Jumatano wiki hii maseneta walimtaka msajili wa ndoa kufika mbele yao na kueleza sababu za kuwepo sheria inayowahitaji wanawake wa kiisilamu kudhihirisha ubikra kabla ya kuozwa na kupewa vyeti vya ndoa.